Wednesday, January 30, 2013

Harusini na Sinta

Mdau wa BLUE PALACE fuatilia kipindi hiki cha Harusini na Sinta ili upate kuona huduma zinazotolewa ndani ya BLUE PALACE plzzzzzzzzzzzzzzzzzzzz Usikose....

HARUSINI NA SINTA NDANI YA BLUE PALACE

Hapa Sinta akiwa ndani ya Saloon  ya Kisasa inayofahamika kama Blue Palace iliyoko maeneo ya Sinza mapambano kwaajili ya kuaandaa kipindicha Television ya DTV kinacholuka hewani kila siku ya Juma nne saa 3:00 usiku
 
Mmmmm....!!!!!! Raha saaaaannnaaaaa mmmmmmmmmmm.......!!!! Hapa Sinta akifanyiwa Message  wakati wa aandalizi ya Kipindi Huku akipata raha na burudani ya Huduma hiyo ........

Monday, January 14, 2013

Tunza Mikono na Miguu yako.



Miguu kama sehemu nyingine za mwili isipoangaliwa vizuri huweza leta madhara kiafya. Ni vizuri miguu ikatunzwa vizuri kuanzia viatu vinavyovaliwa hadi jinsi ya kuisafisha. Kuna aina mbalimbali za viatu mfano viatu vya kufunika vifupi, viatu virefu vya wazi, viatu vifupi vya wazi na viati virefu vya kufunika. Viatu vyote hivi huwa vinakuwa na muundo tofauti kadiri mvaaji anavyopendelea.
Ni vizuri kuepuka kuvaa viatu virefu sana mara kwa mara na hasa kama unatembea navyo kwa muda mrefu maana husababisha matatizo kwenye misuli ya miguu kama vikivaliwa mara kwa mara na kwa muda mrefu. Pia ni vyema kutovaa viatu vya kufunika na vyenye joto sana kwa muda mrefu hasa sehemu zenye joto kali maana huweza leta matatizo kwenye miguu. Vile vile si vyema kuvaa viatu vya wazi nje kama sehemu inabaridi kali na barafu.
Ili miguu yako iweze kuwa na uzuri wa asili siku zote basi ni vizuri angalau mara moja kwa wiki uwe na siku maalumu ya kusafisha miguu yako (sio kwamba siku nyingine husafishi, la hasha hapa naongelea usafi maalum). Andaa maji ya uvuguvugu na uweke nyenye beseni pamoja na sabuni ya maji ambayo ina dawa (medicated).  Kisha kata kucha zako vizuri na kama utapendelea basi uisugue miguu yako kwa kutumia mafuta maalumu ya kusugulia kuanzia kwenye magoti hadi vidoleni (scrub).Kisha loweka kwenye maji kwa muda wa dakika tano.
Baada ya hapo nawa vizuri na kusugua unyayo kwa kifaa maalumu au jiwe laini kisha suuza miguu yako na maji safi. Baada ya hapo kausha vizuri na upake mafuta mazuri kwa ajili ya kulinda ngozi ya miguu. Hakikisha uchafu wote umetoka na hasa kwenye kucha na vidole.
Tunza miguu yako vizuri maana ni zawadi kutoka kwa Mungu.
Mungu akubariki sana.

Sunday, January 13, 2013

Je, Unafahamu Kuhusu Pochi?



Pochi ni sehemu muhimu sana katika maisha ya mwanamke. Pochi zipo za aina, rangi, ukubwa na matumizi mbali mbali. Ni nadra sana kukutana na binti au mama anayetembea bila pochi, na kwa wengine maisha yao yote wanatembea nayo kwenye pochi.
Kuna vitu muhimu ambavyo ni lazima kila mwanamke akumbuke kutembea navyo kwenye pochi, na kuna vingine ni vyema kuwa navyo lakini sio lazima.
Muhimu
1. Pini
2. Sindano na uzi
3. Vifungo
4. Dawa yoyote ambayo unaitumia na kuihitaji
5. Kitambulisho
6. Pedi
7. Kalamu na notebook
Ukipenda
1. Perfume
2. Lip shiner / lip stick
3. Poda
4. Kitana
5. Khanga / mtandio
6. Kadi ya benki
7. Sandals kama unavaa viatu virefu

Thursday, January 10, 2013

Five Kali











Wow!


Huyu ni moja ya wadau na mteja wa BLUE PALACE akiwa ndani ya Saloon ya Blue Palace iliyoko Sinza

Namna bora ya kutunza miguu

Sasa tuzungumzie juu ya utunzaji wa miguu. Miguu ni sehemu inayoangaliwa sana hasa kwa wanawake, kwani unapoamua kuvaa nguo fupi na huku miguu yako haiko katika hali ya kuvutia sina shaka utaanza kujishuku hata kabla ya kutoka nje.
Miguu ni sehemu ambayo inatakiwa kutunzwa kwa kipekee kama ilivyo sehemu nyingine kama uso. Wengi tumekuwa tukipendezesha nyuso zetu na kusahau kbisa habari za miguu.

Haijlishi miguu yako ni miembamba au minene iwapo utaitunza vizuri sina shaka kuwa utavutia kwa nguo yoyote utakayoivaa.
Kuna njia nyingi za kutunza miguu na unaweza kutunza miguu yako hata kama huna fedha za kununulia vikorokoro vinavyotakiwa.
Unaweza kuchukua beseni na kuweka maji ya uvuguvugu yenye povu la sabuni maalum ya kuoshea miguu kisha loweka miguu na iache kwenye maji kwa muda wa robo saa hivi.
Chukua aina ya scrub uliyoichagua kwa ajili ya miguu yako paa na ikikauka anza kusugua miguu yako na hadi kwenye vidole na unyayo.
Kisha jisafishe kwa maji ya uvuguvugu.
Baadhi ya vitu unavyoweza kutumia ili ku kutengeneza miguu yako ni pamoja na foot file, Therapysa virgin vie salt scrub, Pedicure iliyotengenezwa kwa OPI Refresh Cooling ffot Gel, Innoxa cool na Calm liquid talc na Feet first reviving Foot Soak.
Bidhaa hizi unaweza kuzipata kwenye duka kubwa la vipodozi na pia utpata maelezo jisi ya kutumia
Pia unaweza kutembelea baadhi ya saluni ambazo zinatoa huduma hiyo jitahidi hata mara moja kwa mwezi kuhakikisha miguu yako inapata huduma nzuri ili iwe ya kuvutia.
Kwa wale ambao miguu yao ni makovu au madoadoa wajaribu kutumia scrub na kama hawatafanikiwa kuondoa tatizo hilo basi wanashauriwa ktumia cream na sabuni zenye mchanganyiko wa ukwaju kwani

zinasaidia sana kuondoa madoa.
Pia unaweza kuchukua mkwaju ukaloweka kwenye maji ukishalainika changanya mchanganyiko huko na asali kasha paka.
Husaidia kuondoa madao na hata kwa wale wenye ngozi za mafuta na chunusi sugu mafuta yatakauka na chunusi hazitatoka tena.

Wednesday, January 9, 2013

SKIN CARE/JALI NGOZI YAKO

Dry skin care is important as damaged and dry skin needs to receive the proper treatment. Dry skin lotions can help, but there are lots of other things people can do to minimize dry skin and the damage that it does. Here are some effective tips for caring for dry skin.
What Is Dry Skin and How Is It Caused?

Dry skin (or xerosis) has a low level of sebum, which is the skin's natural lubricant. As it does not have enough sebum, it dries out easily and is unable to retain the right amount of moisture needed for healthy skin.

A number of factors may cause dry skin. It is more common in winter when the cold outside and the heat inside contribute in drying up the skin. It can also be caused by hot water or harsh soaps. Poor diet or smoking can also cause or aggravate the problem. Dry skin may also be a symptom of other conditions, including dermatitis, eczema, ichthyoids, psoriasis, an under active thyroid and diabetes. Dry skin becomes more common as people age.

Blue Palace logo

K-LYINN: UREMBO SIO SURA NA MAUMBILE TU

lake halisi ni Jacqueline Ntuyabaliwe, nyota yake ni Sagittarius (Mshale). Wengi bado tunamkumbuka kama mrembo aliyetwaa taji la Miss Tanzania mwaka 2000 na kisha kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya mrembo wa dunia (Miss World) yaliyofanyikia nchini Uingereza na Visiwa vya Maldives.
Tofauti na mawazo ya wengi, kama anavyobainisha katika mahojiano tuliyofanya naye hivi karibuni, alianzia kwenye muziki kisha akaja kwenye urembo na baadaye akaamua kurejea katika muziki mahali ambapo ndipo alipo hivi sasa. Mwezi ujao anatarajia kufyatua albamu yake ya pili itakayokwenda kwa jina la K-Lyinn- Crazy Over You.
Ametoka wapi, nini mtazamo wake kuhusu muziki na urembo, wapenzi wa muziki na mashabiki wake watarajie nini katika albamu yake mpya, nini siri ya urembo wake na anatoa ushauri gani kwa wasichana? Hayo yote na mengineyo ameyaweka bayana katika mahojiano yafuatayo;
BC: Unaweza kuwaambia mashabiki wako kuhusu maisha yako ya utotoni? Unakumbuka nini kuhusu utoto wako?
K-LYINN: Utotoni nakumbuka jinsi nilivyokuwa nacheza na baba akirudi kutoka kazini na mara nyingi alikuwa akinipeleka kutembea jioni.Pia nakumbuka nilivyokuwa nikienda kanisani na mama.Nilikuwa napenda sana kusomewa hadithi za vitabu.
BC: Historia ya maisha yako, kama ilivyoandikwa kwenye tovuti yako, inaonyesha kwamba baada ya shule ulianza shughuli za muziki kwa kuwa mwimbaji wa Tanzanite Band. Baada ya hapo ukaingia kwenye masuala ya ulimbwende ambapo ulifanikiwa kushinda taji la Miss Tanzania mwaka 2000 na kisha baadaye ukarejea kwenye muziki tena. Nini kilivutia kwanza kuingia kwenye muziki na kisha masuala ya ulimbwende?

K-LYINN:
Tokea nilipokuwa na miaka sita au saba nakumbuka nilikuwa napenda sana kuiga na kuimba nyimbo za wanamuziki wa ulaya kama Madonna na Mariah Carey,kwahiyo nilipopata nafasi ya kujiunga na bendi ya Tanzanites kwangu ilikuwa kama njia ya kutimiza ndoto yangu.Kuhusu urembo nakumbuka kuna wakati nilikuwa natamani nipate nafasi ya kuvikwa taji na kuwakilisha nchi yangu lakini sana sana niliamua kushiriki baada ya kukutana na watu mbalimbali ambao walinishawishi nishiriki na kunipa moyo kuwa nina nafasi ya kushinda.
BC: Nini siri ya urembo wako?
K-LYINN: Kwanza kabisa mimi binafsi napenda sana kujipatia muda mrefu wa kupumzisha akili na viungo kila siku na kupata usingizi wa kutosha na ninaamini hiyo ni siri mojawapo ya urembo.Pia huwa nakunywa maji mengi na kula matunda na mboga katika mlo wa kila siku.Nikipata muda huwa nafanya mazoezi.
BC: Miaka zaidi ya sita sasa imepita tangu ulipovishwa taji la Miss Tanzania. Unaweza kutukumbusha kidogo ulijisikiaje siku hiyo?
K-LYINN: Kwanza nilitangazwa kuwa mshindi nakumbuka kuwa nilishikwa na butwaa na ilichukuwa muda kuamini ni mimi niliyeshinda na baada ya kuamini nilijisikia furaha isiyo na kifani.
BC: Mafanikio uliyoyafikia kwenye masuala ya urembo ni ndoto ya wasichana wengi sana.Je pamoja na muziki bado unajishughulisha na masuala ya urembo? Kama ndio kwa jinsi gani na kama hapana, kwanini umeacha?
K-LYINN: Kwa sasa huwa sijishirikishi sana na masuala ya urembo kwanza kwasababu kazi ya muziki inachukua muda wangu mwingi,lakini pia ni kwasababu bado hatuna kazi nyingi sana hapa kwetu zinazohusu urembo.
BC: Unaye mtu yeyote ambaye unamuona kama role model wako? Kwanini?
K-LYINN: Baba yangu ni role model wangu,ni mtu mkarimu na yeye ni daktari na amejitolea maisha yake kusaidia watu.Pia naamini ni baba mzuri sana kwasababu bahati mbaya mama yangu alifariki miaka kumi na mbili iliyopita na baba alinilea vizuri mpaka nimefikia hapa nilipo.Yeye huwa tayari kunisikiliza muda ninapohitaji kuongea nae na huniunga mkono na kunipa ushauri katika maisha yangu.

BC: Sasa naomba tuongelee albamu yako mpya unayotarajia kuitoa hivi karibuni.
Kwanini umeamua kuiita albamu hii K-LYNN?
K-LYINN: Album yangu inaitwa K-LYINN CRAZY OVER YOU,Nimeamua kuuita hivyo kwasababu napenda watu walifahamu na kulizoea jina langu na Crazy Over You ni jina la single itakayokuwepo katika album yangu.

Muonekano wa ndani


Huu ndio muonekano wa ndani ya Blue Palace hapa ni sehem ya mteja kusubiri huduma wakati maandalizi yanafanyika nimoja kati ya Saloon Bomba iliyopo Jijini Dar es salaam maeneo ya Sinza mapambano inayojishughulisha na Issue mbali mbali ikiwemo urembo kwa wakina dada .....nk

Mambo ya Blue Palace


Hii nija kati ya shughuli zifanyikazo BLUE PALACE

Mwandishi auawa katika mazingira ya kutatanisha

MWANDISHI wa Habari wa Kituo cha Redio Kwizera wilayani Kakonko, Mkoa wa Kigoma, Issa Ngumba (45), ameuawa kwa kupigwa risasi na kunyongwa na watu wasiofahamika.
Habari zilizopatikana jana zimeeleza kuwa mwili wa mwandishi huyo ulikutwa porini, siku tatu tangu alipotoweka nyumbani kwake katika mazingira ya kutatanisha.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Frasser Kashai alithibitisha tukio hilo, lakini akasema asingeweza kulizungumzia kwa undani kwa kuwa polisi walikuwa bado eneo la tukio.
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wamesema mwandishi huyo alikutwa jana akiwa amekufa, huku mwili wake ukiwa na majeraha ya risasi na ukiwa umenyongwa na pembeni yake kulikuwa bastola iliyokuwa imetelekezwa pamoja na simu zake mbili za mkononi.
“Mwili wake ulipatikana jana katika Pori la Mlima Kajuluheta ulioko katika Kijiji cha Muhange, Kakonko asubuhi baada ya wananchi kufanya msako wa siku tatu tangu Jumapili iliyopita ikiwa ni siku moja baada ya kupotea katika mazingira ya kutatanisha,” alisema mmoja wa  mashuhuda hao.
Imeelezwa kuwa pamoja  na vifaa hivyo, pia katika eneo hilo la tukio kulikutwa risasi tano na katika mfuko mmoja wa suruali ya marehemu, kulikuwa na noti moja ya Sh10,000.
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Kigoma (KPC) Deogratius Nsokolo alisema: “Sisi ndiyo kwanza tunaelekea eneo la tukio, lakini waandishi wa Wilaya ya Kibondo ambao waliwahi kufika eneo la tukio na kushuhudia uchunguzi wa daktari, wameeleza kuwa marehemu amekufa kwa kunyongwa na kupigwa risasi mkono wa kushoto.”
“Tunaelekea Wilaya ya Kakonko kutoka Kigoma Mjini, lakini daktari amesema maiti inaonekana kunyongwa shingo na kupigwa risasi mkononi.”
Alisema mwili huo ulifanyiwa uchunguzi na daktari Primus Ijumaa wa Hospitali ya Wilaya ya Kibondo.
Kamanda Kashai alisema jeshi lake linasubiri taarifa ya daktari aliyefanya uchunguzi wa mwili wa marehemu pamoja na taarifa za awali za uchunguzi kabla ya kutoa taarifa kamili kwa waandishi wa habari.
Naibu Mhariri wa Kituo cha Redio Kwizera kinachorusha matangazo yake kutoka wilayani Ngara mkoani Kagera, Seifu Upupu alisema mwandishi huyo alipotea tangu Januari 5, mwaka huu saa kumi na moja jioni.
“Simu zake zilikuwa zikiita bila kupokewa kwa muda wote na hadi jana (juzi) zikawa hazipatikani kabisa,’ alisema Upupu na kuongeza:

Karibu Blue Palace