Wednesday, January 9, 2013

K-LYINN: UREMBO SIO SURA NA MAUMBILE TU

lake halisi ni Jacqueline Ntuyabaliwe, nyota yake ni Sagittarius (Mshale). Wengi bado tunamkumbuka kama mrembo aliyetwaa taji la Miss Tanzania mwaka 2000 na kisha kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya mrembo wa dunia (Miss World) yaliyofanyikia nchini Uingereza na Visiwa vya Maldives.
Tofauti na mawazo ya wengi, kama anavyobainisha katika mahojiano tuliyofanya naye hivi karibuni, alianzia kwenye muziki kisha akaja kwenye urembo na baadaye akaamua kurejea katika muziki mahali ambapo ndipo alipo hivi sasa. Mwezi ujao anatarajia kufyatua albamu yake ya pili itakayokwenda kwa jina la K-Lyinn- Crazy Over You.
Ametoka wapi, nini mtazamo wake kuhusu muziki na urembo, wapenzi wa muziki na mashabiki wake watarajie nini katika albamu yake mpya, nini siri ya urembo wake na anatoa ushauri gani kwa wasichana? Hayo yote na mengineyo ameyaweka bayana katika mahojiano yafuatayo;
BC: Unaweza kuwaambia mashabiki wako kuhusu maisha yako ya utotoni? Unakumbuka nini kuhusu utoto wako?
K-LYINN: Utotoni nakumbuka jinsi nilivyokuwa nacheza na baba akirudi kutoka kazini na mara nyingi alikuwa akinipeleka kutembea jioni.Pia nakumbuka nilivyokuwa nikienda kanisani na mama.Nilikuwa napenda sana kusomewa hadithi za vitabu.
BC: Historia ya maisha yako, kama ilivyoandikwa kwenye tovuti yako, inaonyesha kwamba baada ya shule ulianza shughuli za muziki kwa kuwa mwimbaji wa Tanzanite Band. Baada ya hapo ukaingia kwenye masuala ya ulimbwende ambapo ulifanikiwa kushinda taji la Miss Tanzania mwaka 2000 na kisha baadaye ukarejea kwenye muziki tena. Nini kilivutia kwanza kuingia kwenye muziki na kisha masuala ya ulimbwende?

K-LYINN:
Tokea nilipokuwa na miaka sita au saba nakumbuka nilikuwa napenda sana kuiga na kuimba nyimbo za wanamuziki wa ulaya kama Madonna na Mariah Carey,kwahiyo nilipopata nafasi ya kujiunga na bendi ya Tanzanites kwangu ilikuwa kama njia ya kutimiza ndoto yangu.Kuhusu urembo nakumbuka kuna wakati nilikuwa natamani nipate nafasi ya kuvikwa taji na kuwakilisha nchi yangu lakini sana sana niliamua kushiriki baada ya kukutana na watu mbalimbali ambao walinishawishi nishiriki na kunipa moyo kuwa nina nafasi ya kushinda.
BC: Nini siri ya urembo wako?
K-LYINN: Kwanza kabisa mimi binafsi napenda sana kujipatia muda mrefu wa kupumzisha akili na viungo kila siku na kupata usingizi wa kutosha na ninaamini hiyo ni siri mojawapo ya urembo.Pia huwa nakunywa maji mengi na kula matunda na mboga katika mlo wa kila siku.Nikipata muda huwa nafanya mazoezi.
BC: Miaka zaidi ya sita sasa imepita tangu ulipovishwa taji la Miss Tanzania. Unaweza kutukumbusha kidogo ulijisikiaje siku hiyo?
K-LYINN: Kwanza nilitangazwa kuwa mshindi nakumbuka kuwa nilishikwa na butwaa na ilichukuwa muda kuamini ni mimi niliyeshinda na baada ya kuamini nilijisikia furaha isiyo na kifani.
BC: Mafanikio uliyoyafikia kwenye masuala ya urembo ni ndoto ya wasichana wengi sana.Je pamoja na muziki bado unajishughulisha na masuala ya urembo? Kama ndio kwa jinsi gani na kama hapana, kwanini umeacha?
K-LYINN: Kwa sasa huwa sijishirikishi sana na masuala ya urembo kwanza kwasababu kazi ya muziki inachukua muda wangu mwingi,lakini pia ni kwasababu bado hatuna kazi nyingi sana hapa kwetu zinazohusu urembo.
BC: Unaye mtu yeyote ambaye unamuona kama role model wako? Kwanini?
K-LYINN: Baba yangu ni role model wangu,ni mtu mkarimu na yeye ni daktari na amejitolea maisha yake kusaidia watu.Pia naamini ni baba mzuri sana kwasababu bahati mbaya mama yangu alifariki miaka kumi na mbili iliyopita na baba alinilea vizuri mpaka nimefikia hapa nilipo.Yeye huwa tayari kunisikiliza muda ninapohitaji kuongea nae na huniunga mkono na kunipa ushauri katika maisha yangu.

BC: Sasa naomba tuongelee albamu yako mpya unayotarajia kuitoa hivi karibuni.
Kwanini umeamua kuiita albamu hii K-LYNN?
K-LYINN: Album yangu inaitwa K-LYINN CRAZY OVER YOU,Nimeamua kuuita hivyo kwasababu napenda watu walifahamu na kulizoea jina langu na Crazy Over You ni jina la single itakayokuwepo katika album yangu.

No comments:

Post a Comment